Monday, September 3, 2012

MRADI WA " ELIMU YA UJASIRIAMALI MIJINI NA VIJIJINI" WAZINDULIWA JIJINI DAR ES SALAAM

Mwalimu  wa  Ujasiriamali  kutoka  katika  Taasisi  ya  RafikiElimu  Foundation, Mama  Ashankira  Lupembe  , akifundisha  kwa  vitendo  namna  ya  kutengeneza  sabuni   ya  maji. 

Wajasiriamali  wakifanya  "  practical "  ya  kutengeneza  sabuni  ya  maji  kwa  vitendo  mara  baada  ya  kupokea  maelekezo  kutoka  kwa  waalimu  wa  ujasiriamali  kutoka  katika  Asasi  ya  RafikiElimu   Foundation. 

Mwalimu  wa  Ujasiriamali  kutoka  Taasisi  ya  RafikiElimu  Foundation, Mama  Ashankira  Lupembe  akifua  kitambaa  kwa  kutumia  sabuni  iliyo  tengenezwa  wakati  wa  mafunzo  ya  utengenezaji  sabuni   ya  wakati  katika  uzinduzi  wa  mradi  wa  Elimu  ya  Ujasiriamali Mijini  &   Vijijini. 
Mradi uliolenga  kupunguza  tatizo  la  ajira  nchini  kwa  kutroa  elimu  ya  ujasiriamali  kwa  maelfu  vijana  wa  kitanzania  waishio  mijini  na  vijijini  ifikapo  mwezi  Novemba  2014   umezinduliwa  rasmi  leo  jijini  Dar Es  salaam.  Uzinduzi  huo   ulio  fanyika  mapema  leo  katika  eneo  la  Shule  Ya  Msingi  Mlimani  iliyopo  katika  Chuo  Kikuu  Cha  Dar Es  salaam  na  kuhudhuriwa  na  makumi  ya  vijana  wa  kada  mbalimbali  jijini  Dar  es  salaam   uliambatana  na  mafunzo  ya  ujasiriamali   ambapo  wahudhuriaji  walipata  nafasi  ya  kujifunza  kutengeneza  sabuni  za  aina  mbalimbali  kutoka  kwa  wataalamu  wa   kutoka  katika  taasisi  ya  RafikiElimu  Foundation, taasisi  inayo  jihusisha  na  maendeleo  ya  jamii.

Baadhi  ya  wajasiriamali  walio  hudhuria  katika   Uzinduzi  wa Mradi  wa  Elimu  Ya  Ujasiriamali  Mijini  &  Vijijini  uliofanyika   leo  jijini  Dar  Es  salaam. 
Akiulezea  mradi  huu,   mratibu  msaidizi  wa  mradi  huo   alisema   kuwa  mradi  huu  upo    katika  awamu  kuu  mbili.  Awamu  ya  kwanza   itafanyika  kuanzia  tarehe  01  Septemba  2012 hadi  tarehe  29 Septemba  2012, na  utafanyika  katika  mikoa   ya  Dar Es  salaam, Arusha, Mwanza, Mbeya, Morogoro,  Dodoma  na Kilimanjaro, ambapo  mbali  na  kutoa  mafunzo  ya  ujasiriamali, asasi  itatafuta   vijana  kumi  na  wawili  kutoka  katika   hiyo  mikoa  saba   kwa  ajili   ya  kufanya  kazi  kama  wajitoleaji " volunteers"  katika  awamu  ya  pili  ya  mradi  itakayo  anza  rasmi  tarehe 01  Novemba  2012  na   kuchukua  miaka  miwili  hadi    Novemba  2014   ambapo  ndipo  itakapo  kuwa  tamati  ya  mradi  huu.

Awamu  ya  kwanza  ya  mradi  huu  inafanyika  katika  mikoa  ya  Dar  Es  salaam,  Arusha, Morogoro, Kilimanjaro, Dodoma, Mwanza  na  Mbeya.  Jijini  Dar  Es  salaam, mafunzo  yanafanyika  kwa  siku  tatu  kuanzia  tarehe 01  Septemba  2012  hadi  tarehe  04  Septemba  2012  katika  Shule  ya  Msingi  Mlimani  , iliyopo  katika  Chuo  Kikuu  Cha  Dar  Es  salaam...  Ratiba  kamili  ya  awamu  ya  kwanza  ya  mafunzo  haya  ni  kama  ifuatavyo :

1. ARUSHA, MOSHI  & MOROGORO :  Mafunzo  yatafanyika  kuanzia  tarehe  17 hadi  19 Septemba 2012..  Mwisho  wa  kujiandikisha  katika  " programme  hii " kwa  wakaazi  wa  ARUSHA, MOSHI  na  MOROGORO  ni  tarehe  15  Septemba  2012.


Baadhi  ya  wanafunzi  wa  ujasiriamali  waliohudhuria  katika  mafunzo  haya  wakifuatilia  darasa  kwa  makini. 
2. MWANZA, MBEYA   &  DODOMA :  Mafunzo  yatafanyika  kuanzia  tarehe  27 hadi  29 Septemba  2012.
Mwisho  wa  kujiandikisha  katika  programme  hii  kwa  wakaazi  wa  DODOMA, MBEYA  & MWANZA ni  tarehe  25  Septemba 2012.

ORODHA YA MAJINA YA WAJASIRIAMALI WA JIJINI DAR ES SALAAM WALIO JIANDIKISHA KATIKA MRADI WA ELIMU YA UJASIRIAMALI MIJINI NA VIJIJINI.

Yafuatayo  ni  majina   ya   vijana  wa  kitanzania  walio  jiandikisha  katika  awamu  ya  kwanza  ya   Mradi  wa  Elimu  ya Ujasiriamali  Mijini  &  Vijijini  "  EUMIVI   PROJECT. mbao  utaanza  rasmi  siku  ya  jumamosi  ya  tarehe  01  Septemba  2012   kuanzia  saa  nne  kamili  asubuhi  katika  Shule Ya  Msingi  Mlimani  iliyopo  katika  eneo  la  Chuo  Kikuu  Cha  Dar  Es  salaam.  Kwa  jijini  Dar  Es  salaam, mafunzo  yatachukua  siku  tatu, kuanzia  tarehe  01 Septemba  2012  hadi  tarehe 03 Septemba  2012. Baada  ya  hapo mradi  utaendelea  katika  miji  ya Arusha, Morogoro, Mwanza, Mbeya, Dodoma, Tanga  na Shinyanga

          ORODHA   HII  NI    KWA  WAOMBAJI   KUTOKA  JIJINI   DAR ES  SALAAM.

1.  MIRIAM  SYLLERSAID  MZIRAY
2. OTMARY   CHRISPIN  KIOWI.
3. MONICA   ELIAH  NG'ONA.
4.  SHEBA  SHAABAN.
5. FRIDA  EMMANUEL  MUGARULA.
6. AYUB  G.  KAYOMBO.
7.AMIRI  M.  MAGORWA.
8.  FRANK   KAYUMBA.
9.ELIZABETH   PATRICK.
10.   SHEHA   MOHAMED.
11. ROSEMARY  FAUSTIN  MAOKOLA.
12.  MAGRETH   GERWIN  FAYA.
13. DANIEL   A.  SWILA.
14.  MULIMBA  O.  RUYEMBE.
15. MWAJUMA  SHAMTE.
16.  SAMIA  SELEMANI.
17. MWANTUMU  SELEMANI  KALULU.
18. BEATRICE  MIROBO   CHISANYO.
19. HILDEGATH   HAULE.
20.  JOYCE   MAIGE  MGALAGANZA.
21.  DIANNA   R.  MTAITA.
22.LEOKADIA  KINGAMKONO  (  Tafadhali  Tujulishe  namba  yako  ya  simu  haraka  iwezekanavyo )
23.  MUGANYILE  E.  GABRIEL.
24.REHEMA  WILLIAM.
26.  MAGDALENA   R. SHAYO.
27. IBRAHIM  JUMA  OMAR.
28. SOPHIA  SELEMANI  ISSA. ( Tafadhali  tujulishe  namba  yako  ya  simu  haraka  iwezekanavyo O
29.  VICTORIA   ABDALLAH  MPOMA  (  Tafadhali  tujulishe  namba  yako  ya  simu  haraka  )
30. JANETH  ANDREW.
31. LILIAN  BAHATI  (  Tafadhali  tujulishe  namba  yako  ya simu  haraka  iwezekanavyo )
32.  YUSUFU   SAID  JADI.
33. TABU  RASHIDI   LWASSA.
34. MASUMBUKO  MANG'OMBE  JAMES.
35. HELENA  STEVEN  CHACHA.
36. FADHILI  H.  MOTTO.
37. RAMLA  H. MOTTO.
38. PETER  NGWANDU  MASALU.
_______________________________________________


Kwa  ambao  majina  yenu  yame orodheshwa  hapo  juu, mnatakiwa  kufika  katika  eneo  la  Shule  Ya  Msingi  Mlimani  iliyopo  katika  Chuo  Kikuu  Cha   Dar  Es  salaam, siku  ya  Jumamosi  ya  tarehe 01  Septemba  2012  saa   tatu  kamili  asubuhi  kwa  ajili  ya  Uzinduzi  wa Mradi  wa  Elimu  ya Ujasiriamali  Mijini  &  Vijijini "  EUMIVI  PROJECT "  ambapo  mafunzo  rasmi  ya  ujasiriamali katika  mradi  huu  yataanza.

Kufika  katika  eneo  la  tukio  (  Shule  Ya  Msingi  Mlimani )  : Panda  gari  za  Ubungo-Mwenge, mwambie  konda  akushushe  kwenye  kituo  kinaitwa   UDASA ukifika  hapo  UDASA   kama  unatokea  Mwenge  , tazama  upande  wako  wa  kushoto  na  kama  unatokea  Ubungo  tazama  upande  wako  wa  kulia ,utaiona  Shule  Ya  Msingi  Mlimani,  hapo  ndipo  yatakapo  kuwa  yanafanyika  mafunzo  haya..

Unashauriwa  kufika  na kitambulisho  chako,    kalamu  pamoja  na  daftari.  Kamera  hazita  ruhusiwa.

N.B: 1.  Kama  wewe    ni  mkazi  wa  jijini  Dar  Es  salaam,  na  ulituma  maombi  ya  kujiunga  katika  mradi  huu lakini  jina  lako  halionekani  hapo  juu. Tafadhali  wasiliana  nasi  haraka  iwezekanavyo  kabla  ya  tarehe  01  Septemba...
       2.  Kama  kuna  majina  ya  waombaji  kutoka  Dar  Es  salaam  yataongezeka, tutayaweka  hapa  bloguni  kabla  ya  tarehe  01  Septemba  2012.




                          KWA  WAOMBAJI  WA  MIKOANI : 
IFUATAYO  NI   RATIBA  YA   UZINDUZI  WA   AWAMU  YA  KWANZA  YA  MRADI  WA  MAFUNZO  YA  UJASIRIAMALI. MIJINI  & VIJIJINI  KATIKA  MIKOA  YA  ARUSHA, MOROGORO, KILIMANJARO, MWANZA, MBEYA  NA  DODOMA.

Kwa  waombaji  wa  mikoani,  ratiba  ya   awamu  ya  kwanza  ya   mafunzo  haya  itakuwa  kama  ifuatavyo :

                      1.   ARUSHA   ,  MOSHI  NA  MOROGORO
                    Mafunzo  yatafanyika    Tarehe   17, 18  na  19,  SEPTEMBA  2012...


                    2.    MWANZA,  MBEYA  NA   DODOMA
     
                Mafunzo  yatafanyika tarehe  27, 28  na  29, Septmba  2012.

No comments:

Post a Comment