Monday, September 10, 2012

KAMPUNI YA BIA YA SERENGETI YAIPIGA TAFU KIKOSI CHA USALAMA BARABARANI

Kamanda wa Kikosi cha Usalama Barabarani Kamanda Mohamed Mpinga akipokea msaada wa fulana 1000 za kuhamasisha wiki ya usalama barabarani na vipeperushi 500 kutoka kwa mkurugenzi wa mawasiliano wa kampuni ya bia ya Serengeti (SBL) Teddy Mpunda katika makabidhiano yaliyofanyika kwenye makao makuu ya Trafic jijini Dar es salaam, kushoto ni Meneja wa Mipango Endelevu na Uwajibikaji kampuni ya Serengeti Nandi Mwiyombela.
Vifaa hivyo vina thamani ya shilingi milioni 17.5 na kampuni hiyo imesema inaangalia uwezekano wa kuchapisha vipeperushi vingine kwa ajili ya mkoa wa Dar es salaam ambapo hivi vya awali vitapelekwa mikoani
Kamanda wa Kikosi cha Usalama Barabarani Kamanda Mohamed Mpinga akipokea msaada wa vipeperushi 500 kwa ajili ya kuhamasisha wiki ya usalama barabarani kutoka kwa mkurugenzi wa mawasiliano wa kampuni ya bia ya Serengeti (SBL) Teddy Mpunda katika makabidhiano yaliyofanyika mkwenye makao makuu ya Trafic jijini Dar es salaam, kushoto ni Meneja wa Mipango Endelevu na Uwajibikaji kampuni ya Serengeti Nandi Mwiyombela.
Kamanda wa Kikosi cha Usalama Barabarani Kamanda Mohamed Mpingaakizungumza katika makabidhiano hayo wakati alipokuwa akitoa shukurani zake kwa kampuni ya bia ya Serengeti (SBL) wanaofuatia ni mkurugenzi wa mawasiliano wa kampuni ya bia ya Serengeti (SBL) Teddy Mpunda na Meneja wa Mipango Endelevu na Uwajibikaji kampuni ya Serengeti Nandi Mwiyombela.
Mkurugenzi wa mawasiliano wa kampuni ya bia ya Serengeti (SBL) Teddy Mpunda  akizungumza katika makabidhiano hayo kushoto ni Meneja wa Mipango Endelevu na Uwajibikaji kampuni ya Serengeti Nandi Mwiyombela.

No comments:

Post a Comment